Wednesday, 30 October 2013

MAJERAHA YA NAFSI.



MAJERAHA YA NAFSI – UTANGULIZI
Kuna majeraha ya mwili na Majeraha ya nafsi.
Hapa sisemi habara za Majeraha au Vidonda vya ndani ya mwili bali nafsini.
Nafsi kwa sehemu kubwa ni jambo la kiroho; hivyo watu wanapata ugumu mkubwa kuelezea mambo ya nafsi maana ufahamu wa mwilini hawezi kuelezea mambo ambayo ni ya rohoni.
Kimsingi Mungu aliumba mwanadamu akawa na vitu vitatu; Mwili, Nafsi na Roho. Roho na Nafsi ni vitu vigumu kueleweka kwa jinsi ya mwilini ila vinaeleweka kwa jinsi ya rohoni. 1Wathesalonike 5:23. Mungu mwenyewe, Mungu wa amani, awatakase ninyi kabisa, roho zenu, nafsi zenu na miili yenu, nanyi mhifadhiwe kikamilifu bila kuwa na lawama katika Bwana wetu Yesu Kristo. kwa mujibu wa maneno hayo inathibitisha kuwa mtu ni roho,nafsi pamoja na mwili. Ikiwa kasema “Tukaze nafsi” mwili na roho zetu maana yake yote yaani nafsi,Mwili, na Roho vinaweza vikapata shida ikiwa kuna mazingira vikipitishwa kama Mungu anataka kutakasa nafsi zetu, maana yake anataka kuziponya nafsi zetu, kwa hiyo nafsi inaweza ikapata vidonda.
Ukisoma Zaburi 55:4, inasema Moyo wangu unaumia ndani yangu na hofu za maiti zimenizunguka.
Moyo wake au nafsi yake inaumia na asikia ndani yake maumivu na hayo maumivu yamejenga hofu ndani ya moyo wake.
Siku zote Majeraha ya Nafsi huwayanajenga mfumo wa maisha, kwa mfano: Zaburi 55:4 Majeraha yake ya Nafsi yalimjengea hofu au mfumo wa kuishi kwa Uoga. Hofu si mfumo pekee ambao Majeraha  ya Nafsi yanajenga, ipo mifumo mingi na  ambayo hipo kinyume na mfumo wa Ufalme wa Mbinguni.
Mathayo 6:12
Utusamehe deni zetu,kama sisi nasi tulivyokwishakuwasamehe wadeni wetu.
Mfumo wa maisha ya mbinguni unatutaka kuwasamehe wale waliotukosea na kutusababishia Majeraha  ila mtu aliyejeruhiwa Moyo utamjua kuwa ni mgumu kwenye kusamehe maana anaona aliyemkosea hastahili kusamehewa; lakini swali la kujiuliza ni nani katika Wanadamu ambaye amesamehewa na Mungu kwa kusahili? Jibu ni wazi kuwa “Hakuna|”
Ugumu wa kutokusamehe unasababishwa na uchungu, lile fundo la uchungu lililokaa ndani ya moyo kishelia ni uchafu ndani ya moyo;
Maana Biblia inasema Takaseni Nafsi zenu hivyo Wathesolomike 5:23 uondoe uchafu wa moyo ikiwemo uchungu.
Mtu aliyejeruhiwa Moyo maana yake pia amekosa “AMANI” na Mwanadamu hakuumbwa kuishi bila kuwa na Amani kwa hiyo itambidi atafute Amani kwa gharama yeyote ile, au kitu chochote atachofanya na kitampa Amani. Kina Amani za aina nyingi lakini si kila tendo linaweza kumpa Amani ya kweli.
Kina Amani ya Dunia.
Yohana 14:27
“Amani nawaachieni; Amani yangu nawapa niwapavyo mimi sivyo kama Ulimwengu utoavyo.
Hapa tunaona kina Amani ambayo Kristo anampa mtu na kuna Amani ambayo Ulimwengu unapaswa watu,  ni Amani zenye uwezo tofauti ila yenye nguvu ni Amani ya Kristo Yesu.
Badala ya kuingia kwenye vilevi ; kama pombe ili kupata ‘Amani” ni bora ujazwe Roho. Tusilewe kwa mvinyo bali tujazwe Roho ndivyo ushauri wa Biblia.
Ndani ya Roho Mtakatifu kuna Amani ya Kristo inayopita fahamu zote na kuhifadhi mioyo yote Wafilipi 4:6-7
Na Amani ya Mungu ipitayo alali zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.
Maana ya majeraha ya nafsi.
Tumeona kuwa Majeraha ya Nafsi yanajenga mfumo wa maisha ambayo ni kinyume kabisa na ule wa Ufalme wa Mbinguni.
Kwa kujeruhiwa na ama kujijeruhi wewe mwenyewe katika mapito unayopita katika maisha yako ya kila siku. Si kila mtu kajeruhiwa wengine wamejijeruhi wenyewe.
Ukiona kuna jambo ulifanya hata kama ni kipindi cha nyuma lakini ukilikumbuka kama unasikia kulipa kisasi au moyo kuinama au uchungu au unaona hata bora unge…….ujue hiyo ni ishara ya jeraha la nafsi.
Zaburi 39:1-3
Moyo wangu ukawa moto ndani, na katika kuwaza kwangu moto ukawaka; Nilisema kwa ulimi wangu.
Kama aliwaza au kama alikumbuka na moto ukawaka ndani yake maana yake alipokuwa akiwaza akawa anasikia uchungu “Yaaani kwanini nitendewe hivi au vile”
Kama kuna mtu unamkumbuka na kasha unalia au unasikia uchungu ni ishara ya kujeruhiwa moyo.


KAMA UNA MAJERAHA YANAFSI  NA UNAHITAJI  KUFUNGULIWA ,BASI TAMKA MANENO YAFWATAYO  KWAIMANI
NAWE UTAPOKEA UPONYAJI.
Waebrania 11:1-3,Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni udhahiri wa mambo yasiyoonekana. 2Naam, kwa imani baba zetu wa kale walishuhudiwa.
3Kwa imani tunafahamu kwamba ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, vitu vyote vinavyoonekana viliumbwa kwa vitu visivyoonekana.

MAOMBI YA KUTAMKA
Hee MUNGU muumba wa mbingu na nchi  kwajina la yesu kristo mnazareti  kupitia roho mtakatifu ,naomba nisamehewe   dhambi nilizofanya katikamaishayangu, kwamatendo ,maneno na katika kuwaza kwangu kwajina la yesu kristo kupitia roho mtakatifu.Ninakataa  na kuharibu  kumbukumbu za mambo mabaya katika fikra na moyo wangu.   Maumivu yote katika moyo wangu  yatoweke katika jina la yesu kristo kupitia roho mtakatifu ,na damu ya yesu   ifunike moyowangu na maisha yangu katika jina la yesu kristo kupitia roho mtakatifu. Maagano yote ya nguvu zagiza yaliyo wahi kufanyika ama kwa kujua au kwakutokujua  nayaharibu katika jina la yesu kristo kupitia roho mtakatifu ,Bwana yesu futa jialangu katika kitabu cha ukumu na uandike katika kitabu cha uzima amen.

BY MAUMA’MSYANGI ELIKANA (MTUMISHI PAUL MAUMA)
DODOMA –TANZANIA
TEL:0756319013